Nuru FM

Polisi Iringa wamdaka Joseph kwa kumuua mwanaye na kumtupa chooni

6 May 2025, 9:09 pm

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Allan Bukumbi akiwa eneo la tukio. Picha na Ayoub Sanga

Na Adelphina Kutika

Jeshi la polisi mkoni Iringa linamshikilia Joseph Yustino Mhilila mkazi wa mtaa wa Lukosi Kata ya Mtwivila kwa tuhuma za kumuua mtoto wake timotheo Mhulikwa (6) aliyepotea tangu tarehe 1 mwezi wa nne 2025.

Akizungumza na Nuru FM Mwenyekiti wa mtaa wa lukosi Kenedi Mahona anasema ni wiki tatu zimepita tangu mzazi huyo alipotoa taarifa kuwa mtoto wake hapatikani lakini baada ya upelelezi wa jeshi la polisi amekiri kuhusika kwenye mauaji ya mwanae.

Sauti ya Mwenyekiti

Kwa upande wake mmliki wa nyumba alipokuwa akiishi mkazi huyo maximilian luhwago anasema kuwa  kijana huyo alikuwa anajishughulisha na kazi ya usafirishaji bodaboda huku akieleza namna alivyo mpokea mtoto huyo kutoka kwa mzazi mwenzie na kile kilichotokea.

Sauti ya Mmiliki

Nae Afisa usafirishaji Laurent Lukosi ambaye alikuwa wakifanya kazi ya usafirishaji Manispaa ya Iringa amesema kuwa kwa kushirikiana na jeshi la zima moto Mkoa wamefanikiwa kutindua shimo la choo na kukuta vipande vya mwili wa mtoto huyo.

Sauti ya Afisa usafirishaji
Shimo la Choo alilotupwa Mtoto baada ya kuuawa na Baba yake.

Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa SACP Allan Bukumbi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, ambapo ameeleza kuwa  kijana huyo alimkata vipande vipande  mtoto wake na kumtupa katika shimo la choo.

Sauti ya Kamanda
Kijana anayetuhumiwa kumuua Mwanaye.