Nuru FM
Nuru FM
17 April 2025, 11:18 am

Na Zaitun Mustapha na Catherine Soko
Vijana mkoani Iringa wameshauriwa kuwa na mwamko wa kusoma vitabu mbalimbali ili kuweza kukua kiakili, kongeza ufahamu na maarifa.
Hayo yamezungumzwa na baadhi ya vijana Manispaa ya Iringa ambapo wameelezea ni kwa namna gani usomaji wa vitabu umekua na manufaa katika maisha ya kila siku.

Aidha wamesema vijana wengi wanashindwa kwenda Maktaba kuchukua vitabu ili wasome na kupata maarifa na badala yake wanatumia mda mwingi kuperuzi mitandaoni.
Kwa upande wake Kaimu mkutubi wa maktaba ya mkoa Iringa Bi. Elizabeth Rionjo amekiri kuwa vijana wengi hawatumii maktaba kujisomea vitabu ambapo kwa sasa serikali imetoa mwongozo wa mtu mzima kulipia shilingi elfu 10 na wanafunzi shilingi elfu 5 kwa mwaka mzima.
MWISHO