Nuru FM

Bei ya mchele chanzo cha ubwabwa kuuzwa gharama kubwa Iringa

16 April 2025, 11:04 am

Mfanyabiashara wa Mchele akiwa anamuhudumia Mteja. Picha na Geaz Mkata.

Na Geaz Mkata na Rogasia Kipangula

Wafanyabiashara wa Mchele Manispaa ya Iringa wamesema kuwa Bei ya Mchele imepanda kuanzia shilingi 2000 mpaka shilingi 3200 kwa kilo moja.

Wakizungumza na Nuru FM baadhi ya wafanyabiashara wa bidhaa hiyo wamesema kuwa bei hiyo imepanda kutokana na upatikanaji wake kuwa shida kwa sasa hasa baada ya mfungo wa ramadhani Kutamatika.

Sauti ya Wafanyabiashara

Aidha wamesema kuwa Toka mvua zimeanza kusumbua mchele umepanda bei jambo linalopelekea wateja kulalamikia bei kuwa kubwa.

Sauti ya wafanyabiashara

Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara wa chakula Manispaa ya Iringa maarufu MamaLishe wamesema kuwa baada ya mchele kupanda bei wateja wao bado wanataka kuuziwa Wali kwa shilingi 1500.

Sauti ya Wauza chakula