Nuru FM

Wanachuo wahimizwa kujifunza lugha ya Kichina

16 April 2025, 9:51 am

Viongozi Kutoka chuo Cha Mkwawa na Confucius ya chuo kikuu cha Dar es salaam katika picha ya Pamoja. Picha na Joyce Buganda.

Na Joyce Buganda

Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini wametakiwa kujifunza lugha ya kichina kwani  kupitia lugha hiyo  wanaweza kupata fursa mbalimbali ikiwemo ufadhiri katika masomo   yao.

Akizungumza katika mashindano ya taranta za kichina  ya wanafunzi wa vyuo vikuu  duniani  yaliofanyika  katika taasisi ya Confucius chuo Kikuu kishiriki cha elimu  cha Mkwawa RAS wa chuo kikuu Kishiriki cha elimu mkwawa  Prof.  Method Samwel  Semiono amesema kwa chuo cha mkwawa pekee wanafunzi 70 wamejisajili kujifunza lugha hiyo.

Sauti ya RAS

Aidha RAS Semiono amesema taaisi hiyo ilianza rasni mwaka 2013   huku akiwaasa wanafunzi  kutumia fursa ya kujifunza lugha hiyo kwani kuna fursa nyimgi ikiwmo ufadhili wa masomo pindi ukionyeha nia ya kujifunza lugha hiyo.

Sauti ya RAS

Hata hivyo Dr. Musa Hans  ni mwenyekiti kutoka Confucius ya chuo kikuu cha Dar es salaam amesema ni vizuri kujifunza lugha hii kwani lengo kuu ni kujenga madaraja baina ya wanafunzi na makampuni mbalimbali ya kichina ili kukuza ajira nchini.

Sautu ya Musa

Ikumbukwe kilele cha mashindano haya kitafanyika  tarehe 20 mwezi mei katika chuo kikuu cha Dar es salaam na washindi wawili watapata zawadi mbalmbali ikiwa pamoja na kwenda kutembelea nchi ya china.