Nuru FM

Comred Kawaida akagua miradi ya CCM Iringa

11 April 2025, 3:20 pm

Mwenyekiti wa umoja wa vijana UVCCM Taifa komredi Mohamed Kawaida akiwa Mkoani Iringa. Picha na Joyce Buganda

Na Joyce Buganda

Mwenyekiti wa umoja wa vijana UVCCM Taifa komredi Mohamed Kawaida  ameanza ziara ya siku mbili mkoani Iringa lengo likiwa ni kukagua Miradi ya chama pamoja na Kukiimarisha Chama kiwe kwenye umoja na mshikamano hasa katika kipindi Cha kuelekea uchaguzi Mkuu wa 2025.

Akizungumza wakati wa Kuzindua Maduka 11 ya biashara  yaliopo vibanda vya CCM Iringa mjini Komredi kawaida ameipongeza jumuiya ya umoja wa vijana kwa mradi huo kwani kutaongeza mapato katika jumuiya huku amewaasa vijana hao Kuendelea kushikamana pamoja na kudumisha amani katika maeneo yao  kwani vijana ndiyo nguvu ya Taifa.

Sauti ya Kawaida

Awali katibu wa Umoja wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Iringa  Aisha Mpuya amesema mradi huo wa Maduka ni mradi wa umoja wa vijana na wamewapa kipaumbele vijana na wananchi pia ambapo Kuna flemu ilighalimu milioni 6 ambapo milango hii itagharimu shilingi Milioni 2 na nusu kwa mwezi kwa mlango na milioni 4 na nusu hii  kwa mwezi  itagharimu laki 1 na nusu ambapo elfu 50 wanalipa kwa jumuiya  kwa mlango.

Sauti ya Katibu

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa vijana UVCCM mkoa wa Iringa Agrey Tonga amewashukuru vijana kwa ushirikiano wanaonyesha katika mradi huo japo mwanzoni kulikuwa na changamoto  huku akiwaasa kugombea nafasi mbali mbali ifikapo uchaguzi Mkuu  wa mwezi Oktoba  mwaka huu.

Sauti ya Mwenyekiti

Komredi Kawaida ameanza ziara ya siku mbili mkoani Iringa na atatembelea Miradi mbalimbali pamoja na kuzungumza na vijana hii yote ni Kuendelea kukijenga chama Cha Mapinduzi hasa katika kipindi hiki Cha kuelekea uchaguzi Mkuu ifikapo mwezi oktoba mwaka huu.