Nuru FM

Bei ya viazi mviringo Iringa yapaa mwezi April

8 April 2025, 8:22 am

Picha ya muonekano wa Soko kuu Iringa. Picha na Ayoub Sanga

Na Editha Maximillan na Israel Nchimbi

Wafanyabiashara wa zao la Viazi Mviringo katika Soko Kuu Manispaa ya Iringa wamesema kuwa bei ya zao hilo imepanda ikilinganishwa na ilivyokuwa katika mwezi wa Ramadhan.

Wakizungumza na Nuru Fm baadhi ya Wafanyabiashara wa zao hilo katika Soko kuu wamesema kuwa kwa sasa mzunguko wa biashara siyo mzuri ikilinganishwa na kipindi cha mfungo wa ramadhani huku bei ya viazi ikipanda kutoka shilingi elfu 3500 kwa kisado mpaka shilingi elfu 5.

Sauti ya Wafanyabiashara

Aidha Bei ya gunia la viazi kwa sasa inadikia shilingi elfu 65 kwa gunia jambo lililopelekea pia wauzaji kupandisha bei.

Sauti ya Wafanyabiashara

Emanuel  Galala Ni miongoni mwa wanunuzi wa Viazi Mviringo katika soko kuu amesema kuwa viazi viliuzika zaidi katika kipindi cha mwezi wa Ramadhan na kwa sasa upatikanaji wake siyo kama ilivyokuwa wakati huo.

Sauti ya Wanunuzi