Nuru FM

Iringa yaanza kutoa elimu ya kudhibiti ugonjwa wa Mpox

19 March 2025, 12:36 pm

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dr.Silvia Mamkwe akizungumza kuhusu hatua za kukabiliana na Mpox. Picha na Ayoub Sanga

Na Adelphina Kutika

Mkoa wa Iringa umeanzisha kampeni ya kutoa elimu kwa umma ili kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Mpox, ambao umekuwa tishio kwa afya za wananchi.

Akizungumza katika hafla ya kutoa elimu hiyo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Silvia Mamkwe, ameeleza kuwa Mpox ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Mankey Pox na unaambukizwa kwa njia ya kugusana na mtu aliyeambukizwa.

Sauti ya Mganga Mkuu

Kwa upande wake Abubari Chalamila amesema kama viongozi wa dini watahakikisha wanawaelimisha waumini kupitia nyumba za ibada ili kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi

Sauti ya Sheikh

Msaidizi wa Askofu kupitia  Kanisa la KKKT Dayosisi ya Iringa  Askali Mgehekwa amesema kuwa  kama waumini  watashirikiana na vyombo vya habari kuelimisha kuacha kusalimiana kwa kupeana mikono ili kusaidia jamii kuwa salama.

Sauti ya Askofu

MWISHO