Nuru FM

Urusi kuwekeza katika kilimo mkoani Iringa

6 March 2025, 12:47 pm

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba akiwa na Balozi wa Urusi Nchini Tanzania. Picha na Ayoub Sanga.

Na Adelphina Kutika

Balozi wa Urusi nchini Tanzania, Mhe. Andrey Avetisyan, ameonesha dhamira ya kuleta uwekezaji wa viwanda nchini Tanzania, hasa katika sekta ya kilimo, ili kuongeza fursa za ajira na kuchochea maendeleo ya kiuchumi.

Balozi Avetisyan amesema hayo  akiwa ziarani mkoani Iringa, ambapo amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Peter Serukamba na kufanya mkutano  pande hizo mbili na kujadili fursa za kuimarisha uhusiano kati ya Urusi na Mkoa wa Iringa, hususan katika sekta za utalii, kilimo, usafiri na elimu.

Sauti ya Balozi

 Ameongeza kuwa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeweka mazingira bora kwa wawekezaji, jambo ambalo litachochea mataifa mengine kuja kuwekeza kwa wingi.

Sauti ya Balozi

Aidha, Meneja Mkuu wa Browns Tea Plantation, Nashon Kamnyungu, alieleza kuwa ujio wa Balozi Avetisyan ni fursa muhimu kwa upatikanaji wa soko la chai kimataifa na kuongeza thamani ya zao la chai.

Sauti ya Meneja

MWISHO