Nuru FM

Wenezi CCM Wilaya ya Kilolo wapatiwa semina ya kutekeleza majukumu yao

28 February 2025, 8:46 am

Mwenezi wa CCM Mkoa wa Iringa Joseph Lyata akizungumza katika semina Wilaya ya Kilolo. Picha na Joyce Buganda

Na Joyce Buganda

Kuelekea uchaguzi mkuu mwezi oktoba mwaka huu makatibu, siasa, uenezi na mafunzo w CCM ngazi ya kata na matawi  wilayani kilolo ukanda wa juu wamepewa semina elekezi ili kuwaandaa na kuwakumbusha kutekeleza majukumu yao Kulingana na katiba na Kanuni za Chama hicho na kuelewa mipaka yao ya kazi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chama cha mapinduzi CCM wilaya ya kilolo, Katibu siasa, Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Iringa Joseph Lyata amesema makatibu uenezi wana wajibu wa kuhakikisha heshima ya chama inatunzwa vyema.

Sauti ya Ryata

Naye Mbunge wa Jimbo la Kilolo Justin  Nyamoga amewatoa rai kwa wenezi kuhakikisha miradi iliopo kwenye maeneo yao ya utawala inalindwa na kusimamiwa ipasavyo pamoja na kukisema vyema Chama Cha Mapinduzi.

Sauti ya Mbunge

Hata hivyo katibu siasa na uenezi wilaya ya kilolo Reminius Sanga amesema ukanda wa juu wa kilolo una makatibu wenezi wa matawi na kata 83 amaamini semina hiyo imewaingia na anaamini  wanakwenda kuwafikishia wananchi wa maeneo yao  ujumbe.

Sauti ya Sanga

Semina hiyo imekuwa chachu kwa Waenezi hao kuwa Mstali wa mbele kukisemea Chama, kuitaja na kuielezea Miradi Mikubwa ya Maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya CCM ili Wananchi wawe na uelewa wa namna Fedha zinavyotumika Kutatua kero, vilio na Changamoto zinazowakabili.

MWISHO