Nuru FM

Bilioni 11.7 kutengeneza barabara za Mafinga Mji

4 February 2025, 9:33 am

Baadhi ya madiwani Mafinga Mji wakifuatilia taarifa za taasisi za serikali. Picha na Hafidh Ally

Na Hafidh Ally

Halmashauri ya Mji Mafinga Mkoani Iringa imeomba kupatiwa Bilioni 11.7 kwa ajili ya matengenezo ya barabara korofi katika jamii.

Hayo yamezungumzwa na  Meneja wa Wakala wa barabara vijijini (TARURA) Wilaya ya Mufindi Mhandisi Richard Sanga wakatia akitoa ripoti ya utekelezaji wa bajeti ya TARURA katika kikao cha Baraza la Madiwani cha kupitisha bajeti ya mwaka 2025/2026 na kuongeza kuwa fedha hizo zitaweza kutatua kero ya ubovu wa moundombinu ya barabara Mafinga Mji.

Sauti ya Mhandisi

Akichangia hoja hiyo Diwani Kata Ya Saohill, Mheshimiwa Denis Kutemile ameiomba Tarura kuboresha miundombinu ya barabara ili huduma za kijamii ziweze kufikiwa.

Sauti ya Diwani Saohili

Naye Mwenyekiti Wa Halmashauri Ya Mji Mafinga , Mheshimiwa Regnant Kivinge ameitaka Tarura kuhakikisha bajeti iliyopendekezwa inatatua changamoto zote za barabara kwani wana imani na utendaji kazi ambao wameuonesha katika mji huo.

MWISHO