Nuru FM

Mzabuni atekelekeza mradi wa nyumba ya mwalimu Ndolezi

22 October 2024, 11:01 am

Mhe.Justis Kisoma Diwani wa Kata ya Boma Halmashauri ya Mji Mafinga Akizungumzia kuhusu mradi huo. Picha na Fredrick Siwale

Na Fredrick Siwale

Wananchi wa Mtaa wa Ndolezi uliopo Kata ya Boma Halmashauri ya Mji Mafinga wameiomba Serikali kuwatumia wazabuni wa ndani kusimamia miradi ya maendeleo ili kuepukana na ucheleweshaji wa kukamilisha Miradi.

Hayo yamezungumzwa na baadhi ya wananchi wa Mtaa huo kufuatia kusimama kwa mradi wa Ujenzi wa  nyumba ya Mwalimu wenye thamani ya shilingi milioni 100 baada ya kutelekezwa na Mkandarasi   zaidi ya  miezi miwili na kutokomea kusiko julikana.

Sauti ya Wananchi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Tawi la Ndolezi Bw. Lenard Chavala amesema kuwa kinachosababisha zoezi la ujenzi wa jengo hilo ni kutokuwa na fedha za kuendesha zoezi hilo huku wakiiomba serikali kumtafuta mkandarasi ili kumalizia jengo hilo.

Sauti ya Mwenyekiti

Mhe.Justis Kisoma Diwani wa Kata ya Boma Halmashauri ya Mji Mafinga amesema mradi wa nyumba ya Mwalimu Shule ya Sekondari Ndolezi ambao unadaiwa kutelekezwa upo  Halmashauri ya Mji Mafinga Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa .

Mhe.Kisoma amesema mradi wa nyumba ya Mwalimu ya two in one ulianza Ujenzi wake Agosti 05,2024 na ulipaswa kuwa umekamilika  Oktoba 18, 2024 mwaka huu.

Sauti ya Diwani Kisoma

Mwenyekiti wa kamati ya bodi ya Shule ya Sekondari Ndolezi Bi.Hongera Swenya ambaye ndiye msimamizi wa Shule  pamoja na Afisa elimu Sekondari Halmashauri ya Mji Mafinga Stephen Shemdoe hawakuwa tayari kuzungumza sakata hilo.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji  Halmashauri ya Mji Mafinga Bi.Fedelica Myovella alipotafutwa kwa njia ya simu yake ya mkononi alidai atafuatilia mwenendo wa ujenzi wa jengo hilo.   

Mkandarasi aliyetekeza mradi huo aliyefahamika kwa jina la Hamisi Mkurupale tayari amekwishalipwa kiasi cha shilingi milioni 5.3 kati ya shilingi milioni 100 alizotakiwa kulipwa.