Nuru FM

Mapesa: Miundimbunu bora ya shule fursa kwa watoto kusoma

4 September 2024, 12:13 pm

Mapesa Makala akizungumza kuhusu miundombinu ya Shule inavyosaidia Wazazi kupeleka watoto wao shule. Picha na Furahin Kahise

Na Joyce Buganda

Wazazi na walezi wa kijiji cha Kisilwa Kata ya Mahuninga Wilaya ya iringa wamepongezwa kwa kuwa na muamko wa kuwaendeleza watoto wao shule pindi  wanapomaliza  darasa la saba.

Hayo yamezungumzwa kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha kisilwa na Afisa tarafa wa Idodi Makala Mapesa na kuongeza kuwa kipindi cha nyuma wazazi walikuwa wanawaozesha watoto wao mara baada ya kumaliza darasa la saba lakini baada ya serikali kuboresha moundombinu ya shule wazazi wamekuwa na mwamko wa kuwapatia elimu watoto wao.

Sauti ya Mapesa

Naye Diwani wa kata ya mahuninga Benitho kisogole amesema Zaidi ya shilingi bilioni 1 zimeletwa kwenye kata hiyo kwa ajili ya miradi ya  maendeleo ikiwemo elimu.

Sauti ya Benitho

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu  wa Shule ya Sekondari Makifu Jailos Mwakavindi amesema  shilingi million 260 zimeletwa shuleni hapo kwa ajili ya ujenzi wa bweni pamoja na ujenzi wa vyoo.

Sauti ya Mkuu wa shule

MWISHO