Nuru FM

Mradi wa HEET kutatua changamoto ya upungufu wa hosteli MUCE

3 September 2024, 9:33 am

Mkurugenzi  wa Kampuni ya Kitanzania ya Dimetoclasa Real Hope Limited and Mponera Construction Dickson Mwipopo akiwa katika hafla ya utiaji saini mkataba mradi wa HEET. Picha na Adelphina Kutika

Ukosefu wa hosteli katika kada za elimu hapa nchini Tanzania imekuwa ni changamoto inayowakabili wanafunzi wengi jambo linalopelekea kushindwa kutimiza malengo yao.

Na Adelphina Kutika

Wanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE) wameishukuru serikali kuwaletea mradi wa (HEET) unaokwenda kutatua changamoto  ya ubakaji na wizi kwa wanafunzi wanaoishi nje ya hosteli.

Wakizungumza kwa niaba ya wanafunzi Rais wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE) Steven Mgalla na Makamu wake Remisha Gastoni  Milazi  mara baada ya hafla ya utiaji saini mikataba  ya ujenzi  wa majengo manne kupitia mradi wa elimu ya juu kwa mageuzi ya kiuchumi (Heet) wenye thamani ya shilingi bilioni 14.8 na kampuni ya Kitanzania ya Dimetoclasa Real Hope Limited and Mponera Construction wamesema wanafurahishwa na mradi huo kwa sababu unakwenda kuwasaidia kupata hosteli .

Sauti ya Wanafunzi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa(MUCE) Prof. William Anangisye amesema kuwa  mradi huo unakwenda kuchangia katika maeneo muhimu ya uvumbuzi, maendeleo ya kiuchumi na umuhimu wa soko la ajira, kwa kuwekeza katika miundombinu inayohitajika kwa ufundishaji na utafiti wa kisasa .

Sauti ya Prof. Anangisye

Rais wa chuo hicho Prof. Deusdedit Rwehumbiza amesema mradi huu unakwenda kutatua changamoto kubwa zaidi ya hosteli  kwa wanafunzi takribani 6,200.

Sauti ya Prof. Rwehumbiza

Dickson Mwipopo ni mkurugenzi  wa kampuni ya Kitanzania ya Dimetoclasa Real Hope Limited and Mponera Construction  ameomba viongozi kuhakikisha wanatoa kazi wazawa kwa asilimia100 ili kuongeza uchumi wa taifa letu na kuongeza fursa za ajira kwa vijana.

Sauti ya Mwipopo

MWISHO