Nuru FM

Manispaa ya Iringa yapata hati safi ripoti ya CAG

19 June 2024, 10:30 am

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba akizungumzia kuhusu ripoti ya CAG. Picha na Adelphina Kutika

Wakati Mikoa mingine ikiwa na hati yenye mashaka kuhusu ukaguzi kwa hesabu za serikali, Manispaa ya Iringa imezidi kufanya vizuri katika hesabu zake kwa mwaka uliopita.

Na Adelphina Kutika

Mkuu wa Mkoa wa Iringa  Mhe. Peter Serukamba amepongeza Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kwa kupata Hati safi za Ukaguzi kwa hesabu  zilizoishia tarehe 30 Juni, 2022/2023.

Serukamba ameyasema hayo wakati wa Mkutano wa Baraza Maalumu la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ya  kujadili Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2022/23. 

Sauti ya Serukamba

Aidha Serukamba ameiagiza halmashauri ya manispaa ya iringa kuwachukulia hatua za kisheria watumishi waliosababisha kuibuliwa kwa hoja zisizo za msingi katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) zinazohusu masuala ya ubadhirifu wa fedha.

Sauti ya Peter

Diwani wa kata ya Ruaha Tandes Sanga amemuomba mkuu wa Mkoa kutenga siku maalumu na kufanya Kikao cha ndani ili kujadili kwa kina hoja za CAG.

Sauti ya Diwani Sanga

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada amesema wamejipanga kuhakikisha wanafanya vikao vitakavyoleta suluhu ya utekelezaji bora wa miradi.

Sauti ya Meya Iringa

MWISHO