Nuru FM
Nuru FM
10 April 2026, 08:43

Na Fredrick Siwale
Wafanyabiashara wa Soko la Mashujaa Halmashauri ya Mji Mafinga wameiomba serikali kuwapatia Mikopo ili waweze kukuza mitaji yao.
Akizungumza na Nuru FM Mwenyekiti wa Soko la Mashujaa Bw. Devick Kihindo amesema kuwa wajasiriamali wengi wanatamani kupata mikopo ila bado hawajajua utaratibu wa kunufaika nayo.
Naye Diwani wa Kata ya Boma Mh. Baraka Kisakanike Amekiri kuwepo kwa changamoto ya Mitaji kwa wajasiriamali wengi huku akibainisha kuwa tayari serikali imeweka utaratibu wa kunufaika na mikopo ya Halmashauri.

Naye Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini Mh. Dickson Lutevele VILLA amesema kuwa wanaotaka mikopo lazima wawe kwenye vikundi vilivyosajiliwa na kwa kuwa wapo katika maeneo ya biashara watapewa kipaumbele.
Aidha Mh. Villa amesema kuwa baadhi ya wajasiriamali wanaogopa kufuata utaratibu wa kuchukua Mikopo ya Halmashauri na badala yake wanachukua mikopo ya kausha damu ambayo inakuja kuwaletea shida hapo baadaye.