Nuru FM

Wananchi Ng’uruhe wajengewa machinjio ya kisasa

10 April 2026, 09:09

Mwenyekiti wa Shirika la African Exchange Development Mwalimu Shadrack Nyaulingo akiwa na wenyeji wake. Picha na Joyce Buganda

Machinjio hiyo imetajwa kuwa msaada katika kuzingiatia afya za wananchi wa Kijiji hicho.

Na Joyce Buganda

Wananchi wa kijiji cha ng’uruhe Kilichopo wilaya ya kilolo wameshukuru shirika la African Exchange Development  kwa kujengewa machinjio ya kisasa  itayorahisisha shughuli za uchinjaji wa nyama.

Wakizungumza na kituo hiki  baadhi ya wananchi  wa kijiji hicho wamelishukuru shiriki hilo kwa kuwaletea machinjio hayo ya kisasa kijijini hapo ambapo awali hawakuwa na  machinjio rasmi jambo lililohatarisha usalama wa afya zao.

Sauti ya Wananchi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa  Mipango  na Fedha wa kijiji cha ng’uruhe Bw. Israel Magelenge amesema hapo awali walikuwa wanakabiliwa na ukosefu wa sehemu salama na yenye viwango bora vya uchinjaji hali iliokuwa ikiathiri ubora wa nyama pamoja na afya  kwa walaji.

Sauti ya Mwenyekiti

Naye Mwenyekiti wa Shirika la African Exchange Development Mwalimu Shadrack Nyaulingo amesema mradi huo ni sehemu ya juhudi za kuboresha maisha ya wananchi kupitia miradi ya maendeleo inayogusa mahitaji ya msingi  ya jamii.

Machinjio hayo Yanatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya uchumi kwa wakazi wa ng’uruhe hasa kwa wafugaji na na wafanyabiashara wa nyama huku wakichangia pia kuboresha hali ya afya kwa jamii kwa ujumla.