Nuru FM
Nuru FM
25 March 2026, 10:16 am

Mpango huu unalenga kuhakikisha kila kipande cha ardhi nchini kinapimwa ili kumwezesha mmiliki kuwa na haki mbalimbali zinazoambatana umiliki wa ardhi.
Na Telesia Chalamila
Wananchi wilaya ya Iringa wametakiwa kurasimisha umiliki wa ardhi zao ili kupunguza migogoro ya ardhi na kuongeza thamani yake.
Hayo yamezungumzwa na Mkuu wa Idara ya ardhi Halmahauri ya Wilaya ya Iringa Bw. Geofrey Kaluwa na kuongeza kuwa hatua za urasimishaji ardhi inasaidia utambuzi wa kipande cha ardhi.

Naye Afisa Mipango Miji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Calist Mushi ameeleza kuwa ni vyema kabla ya wananchi kuuza kiwanja wahakikishe wanapata miongozo kutoka katika vyombo husika.
Awali Mpima ardhi kutoka Halmahauri hiyo Jesse Josephati amebainisha kuwa maeneo yenye huduma za kijamii kama barabara na hospitali ni moja ya maeneo muhimu ambayo huanza katika utambuzi ili kurasimishwa.
