Nuru FM

DC Sitta aagiza barabara ya Kitasengwa kutengenezwa

24 March 2026, 9:12 am

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Benjamini Sitta akizungumza na wananchi wa Kitasengwa. Picha na Hafidh Ally

Barabara hiyo ilihabirika kutokana na Mvua zinazoendelea kunyesha mkoani Iringa.

Na Hafidh Ally

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Benjamin Sitta amewataka maafisa wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kushughulikia changamoto ya uharibifu wa miundombinu ya barabara katika  Mtaa wa Kitasengwa, Kata ya Isakalilo, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ili kurejesha mawasiliano na shughuli za wananchi.

Mh. Sitta ametoa maagizo hayo mara baada ya kutembelea eneo hilo lililoathirika na kuongeza kuwa ni vyema Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, kupitia vikao vyake vya maendeleo, kuona umuhimu wa wa kutambua na kusajili barabara hizo ili kuiwezesha Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kuanza rasmi matengenezo ya miundombinu hiyo.

Sauti ya DC Sitta

Naye Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Barnabas Jabir amesema kuwa watashirikiana na wananchi wa eneo hilo kuhakikisha barabara hiyo inapitika.

Sauti ya Meneja TARURA

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Kitasengwa wameishukuru serikali ya Wilaya ya Iringa kwa kufika na kujionea hali ya barabara hiyo huku wakiiomba iweze kutatuliwa kwa ubora zaidi.

Sauti ya Wananchi

Katika siku za hivi karibuni, Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Benjamin Sitta, amekuwa akifanya ziara za mara kwa mara katika maeneo mbalimbali yaliyopata madhara ya viwango tofauti kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha katika wilaya ya Iringa.