Nuru FM

Samia ardhi kliniki kutatua migogo ya ardhi

7 March 2026, 10:41 am

Wataalamu wa ardhi wakiendelea na majukumu yao katika kliniki ya ardhi iringa Mjini. Picha na Telesia Chalamila

Kliniki hii ina lenga kuhakikisha wanawake wanapata fursa ya kumiliki ardhi sawa na wanaume.

Na Telesia Chalamila na Elika Matonya

Kuelekea maadhimisho ya siku ya Wanawake  Duniani  Wizara ya ardhi nyumba na Maendeleo ya Makazi Ofisi ya ardhi Mkoa wa Iringa imeandaa kliniki maalumu ya ardhi ijulikanayo kama samia ardhi kliniki kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto za ardhi zinazowakabili wananchi hususani wanawake.

Akizungumza na Nuru FM Josefer Mwenda Msajili wa ardhi Msaidizi Mkoa wa Iringa amesema kuwa Samia Ardhi Kliniki imeandaliwa rasmi kwa lengo la kutatua migogoro ya ardhi ikiwa ni pamoja na masuala ya umiliki wa hati.

Sauti ya Mwenda

Bi  Flora shija Afisa ardhi Mkoa ameeleza kuwa wameamua kuweka kliniki ya ardhi kwa lengo la kusaidia kukuza ongezeko la wanawake wanao miliki hati Tanzania na pia ameshauri jamii kwa ujumla kuzingatia haki na usawa.

Sauti ya Flora

Nae mnufaika katika kliniki hiyo, Bi Tusajigwe Emmanuel na mmiliki wa ardhi Manispaa amesema kuwa amenufaika na kliniki hiyo kwani ameishi mda mrefu  bila hati lakini kupitia Samia ardhi  kliniki imemsaidia kuwa mmiliki halali  wa eneo lake.

Sauti ya Mnufaika