Nuru FM

Kadi ya alama kuongeza malezi kwa mtoto

5 March 2026, 5:16 pm

Wawezeshaji wa mafunzo ya utekelezaji wa mradi wa PJT–MMMAM wakitoa maelekezo kwa waratubu wa afua tano za mradi huo Manispaa ya iringa. Picha na Adelphina Kutika

Mafunzo hayo yatasaidia kujua mfumo wa kupata takwimu halisi katika maendeleo ya ukuaji wa mtoto.

Na Adelphina Kutika

Waratibu wa afua tano zinazotekeleza mradi wa PJT–MMMAM katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wamepatiwa mafunzo ya siku moja kuhusu ujio wa Kadi ya Alama ya Malezi na Makuzi ya Mtoto (SCORECARD), mfumo mpya utakachosaidia kuboresha ufuatiliaji wa huduma za malezi na maendeleo ya awali ya mtoto.

Akizungumza katika  mafunzo yaliyoratibiwa na Mtoto kwanza  mkoa wa Iringa Shirika la Developmentof Youth Disable and Children Care (IDYDC), Afisa Ustawi wa Jamii Hamza Shemweta muwezeshaji wa mafunzo, amesema lengo ni kuwajengea uwezo waratibu hao kuielewa kadi hiyo namna itakavyofanya kazi, kukusanya na kuchambua takwimu sahihi za watoto.

Sauti ya Hamza

Kwa upande wake, Mratibu wa PJT–MMMAM Mkoa wa Iringa, Martine Chuwa, amesema ujio wa Kadi ya Alama umekuwa chachu ya kuboresha utoaji wa huduma kwa watoto na sasa wadau wataweza kujipima kwa kutumia takwimu sahihi na viwango vinavyoeleweka.

Sauti ya Chuwa

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo ikiwamo,Clous Kayombo Afisa Lishe kutoka Manispaa ya Iringa, amesema mafunzo hayo yameboresha utendaji kazi wao na kuimarisha ushirikiano miongoni mwa wataalamu wa sekta mbalimbali wanaohusika na malezi ya mtoto.

Sauti ya Kayombo

Hata hivyo uanzishwaji wa Kadi ya Alama ya Malezi na Makuzi ya Mtoto unatarajiwa kuleta mapinduzi katika ukusanyaji na matumizi ya takwimu, na hivyo kusaidia kupanga na kutekeleza mipango madhubuti ya kuboresha ustawi wa watoto.