Nuru FM

Mwaipopo kumalizia nyumba ya jumuiya ya wazazi Mufindi

28 January 2026, 12:48 pm

Viongozi katika meza kuu kwenye kikao cha Jumuiya ya wazazi Mufindi. Picha na Fredrick Siwale

Nyumba hii itasaidia viongozi wa jumuiya hii kukaa sehemu salama na kutekeleza majukumu ya Chama.

Na Fredrick siwale

Mjumbe wa mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Mufindi Ndg. Dickison Mwipopo ameahidi kugharamia umaliziaji wa ujenzi wa nyumba ya Katibu wa Jumuiya hiyo. 

Akifungua Kikao cha Jumuiya ya Wazazi Wilaya Ndg. Dickison Mwipopo, amesema atagharamia kwa kutoa mbao za upauaji, mabati na kupiga lipu jengo hilo ambalo limefikia hatua ya Boma.

Sauti ya Mwaipopo

Ndg. Mwipopo amewataka Wazazi Wilayani humo kujenga tabia ya kuwalea Watoto wao katika malezi bora ili kuwaepusha na matukio ya ukatili kwa faida ya Jamii na Taifa kwa ujumla.

Awali Aidha akitoa semina Mwenyekiti wa SMAUJATA Mkoa wa Iringa Bi. Rehema Mbedule alionyesha kusikitishwa na vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii ikiwemom wanawake kuwapiga waume zao.

Sauti ya Rehema

Amesema kuwa matukio ya wanaume kupigwa na wake zao yameripotiwa zaidi jambo ambalo wanaungana na mamlaka nyingine kukemea.

Sauti ya Rehema

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Ndg. Festo Kilipamwambu alimshukuru Mgeni rasmi Ndg. Mwipopo kwa kuwa na moyo wa Uzalendo na vitendo kwa chama cha Mpinduzi CCM.