Nuru FM

RC Kheri ataka usimamizi bora wa miradi

15 January 2026, 11:08 am

Mkuu wa Mkoa wa Iringa akizungumza katika ziara yake Wilaya ya Mufindi. Picha na Ayoub Sanga

“Mimi sipendi kuona miradi ya maendeleo inasimamiwa kwa kusuasua” RC Kheri

Na Ayoub Sanga

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Kheri James ameagiza kuimarishwa kwa ufuatiliaji na usimamizi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa mkoani Iringa ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati, kwa ubora na kwa kuzingatia thamani ya fedha.

Mhe. Kheri ametoa agizo hilo wakati wa ziara za ukaguzi wa miradi ya maendeleo Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, ambapo amebaini kusuasua kwa mradi wa ujenzi wa shule ya awali na msingi unatokelezwa kupitia shule ya Sekondari Ngwazi kutokana na ukosefu wa vifaa vya ujenzi hususani vigae, licha ya kuwepo kwa mafundi pamoja na fedha za utekelezaji wa mradi huo.

Sauti ya Kheri RC Iringa

RC Kheri James amesema kuwa ni jambo lisilo na mantiki kuona mradi unakwama kwa kukosekana kwa vifaa ilhali fedha zipo na mafundi wapo tayari kufanya kazi.

Sauti ya Kheri RC Iringa

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa vifaa vyote vya ujenzi vinapatikana mara moja na miradi yote iliyokuwa imekwama kuanza kutekelezwa haraka sana.