Nuru FM

Iringa kuadhimisha miaka 20 ya Mahakama

8 December 2025, 8:49 pm

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kheri James akizungumza na waandishi wa habari. Picha na Joyce Buganda

Kauli mbiu ya Mahakama ya Tanzania Kanda ya Iringa inasema siku zote ni uadilifu  ueledi na uwajibikaji.

Na Joyce Buganda

Ikiwa tupo katika wiki ya maadhimisho ya miaka 20 ya mahakama Kuu Tanzania kanda ya Iringa, Wananchi Mkoani Hapa wametakiwa kujifunza mambo ya kisheria, haki na kimahahama.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh. Kheri James amesema  maadhimisho hayo yanaanza Leo tarehe 8/12/2025 kwa kuanza na vipindi vya radio na televisheni na kilele chake kitafanyika 15/12/2025.

Sauti ya Rc

Rc kheri amesema umuhimu wa miaka 20 kwa kanda ya Iringa ni ushuhuda safari ndefu wa kazi zinazofanyika kama kurahisisha utendaji kazi wa kimahakama,   matumizi ya tehama kuongeka kwa majaji na watumishi.

Sauti ya Kheri

Hata hiyo DC kheri amesema mahakama serikali imeendelea kushirikiana na mahakama kama muhimili wa dola masuala ya kiusalama miundombimu , kutoa maeneo ya ujenzi wa vituo vya mahakama ya mwanzo katika mkoa wa Iringa  hiyo yote ni kwa mujibu wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania

Sauti ya Rc