Nuru FM

Madiwani Mufindi DC waaswa kukusanya mapato

3 December 2025, 1:43 pm

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama Wilaya ya Mufindi Mh. Benedict Nkomola Akiwa katika Baraza la madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi. Picha na Fredrick Siwale

“Ukusanyaji wa mapato utasaidia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo”

Na Fredrick Siwale

Madiwani wa Baraza jipya la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, wamekula kiapo cha utii na uwajibikaji kwa kipindi cha mwaka 2025 hadi 2030.

Kiapo hicho kimesimamiwa na Mhe. Benedict Nkomola, mbele ya Dkt. Linda Salekwa Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Bw. Ruben Chongolo Katibu Tawala wa Wilaya na Mashaka mfaume Mkurugenzi Mtendaji wa wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi.

Baada ya kiapo hicho Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Dkt. Linda Salekwa , amewataka Waheshimiwa Madiwani hao kwenda kuwaletea Wananchi maendeleo kwa kuibua vyanzo Vipya vya mapato.

Sauti ya DC Linda

Dkt. Salekwa amesema ufike wakati ambao fedha za mapato za Vikundi na maendeleo yake zipatikane kupitia miradi mipya inayobuniwa tofauti na ilivyo hivi sasa.

Sauti ya DC Linda

Akizungumza baada ya kula kiapo cha Utiifu Diwani wa Kata ya Makungu Felix Lwimbo amesema kuwa atahakikisha anafanya kazi kwa bidii kuwatumikia wananchi kwani tayari amesimamia utekelezaji wa miradi ya Bilion 5.6 katika kata yake.

Sauti ya Diwani