Nuru FM

Kamanzi: Andikeni habari zenye tija kuelekea COP 30

28 October 2025, 12:34 pm

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Media Foundation Dkt. Dastan Kamanzi akizungumza na wanahabari. Picha na Joyce Buganda

“Lengo la mafunzo hayo ni kuwaona wanahabari katika ngazi ya kitaifa wakiweza  kuhabarisha jamii juu ya mkutano huo kwa kuandika habari za kabla, wakati na baada ya mkutano”

Na Joyce Buganda

Wanahabari wametakiwa kuandika habari zenye kufikia jamii  hasa katika kipindi hiki     kuelekea mkutano wa umoja wa mataifa wa mabadiliko ya tabia nchi (COP 30) unaotarajiwa kufanyika  kuanzia tarehe  10 mpaka tarehe 21 mwezi Novemba mwaka 2025 katika mji wa Belem nchini Brazil.

Akizungumza baada ya mafunzo ya siku 3  kwa wanahabari 20 kutoka  mikoa 13   ya Tanzania bara yaliofanyika katika hotel ya PH  EXECUTIVE iliyopo mjini Morogoro Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Media Foundation Dkt. Dastan Kamanzi amesema  wanatamani kuona uandishi wenye Tija katika vyombo vya habari hasa katika suala la mabadiliko ya tabia nchi.

Sauti ya Kamanzi

Awali Meneja Muwezeshaji kutoka shirika la Climate Action Network Tanzania Boniventure Mchomvu amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwaona wanahabari katika ngazi ya kitaifa wakiweza  kuhabarisha jamii juu ya mkutano huo kwa kuandika habari za kabla, wakati na baada ya mkutano.

Sauti ya Boniventure

Nao baadhi ya wanahabari waliopata mafunzo hayo wamesema mafunzo hayo yamekuwa nguzo muhimu watafahamu mengi zaidi kimataifa yatakayozungumzwa katika mkutano huo wa COP 30 na kulinganisha na mambo ya nchini Tanzania ambayo yatamgusa hata mwananchi wa chini katika sekta ya mabadiliko ya tabia nchi.

Sauti ya Wanahabari

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Tanzania Media Foundation (TMF) kwa kushirikiana na Oxford policy Management (OPM) kwa ufadhili wa Ubalozi wa nchi za Uingereza na Uswisi.