Nuru FM

Abiria waaswa kukata Tiketi halali za Mabasi

23 October 2025, 10:25 am

Maafisa wa Usalama barabarani wakiwa katika kipindi cha Nyambizi Nuru FM. Picha na Azory Orema

Na Noela Nyalusi

Jeshi la Polisi Kikosi Cha usalama Barabarani Mkoa wa Iringa limewataka abiria wanaosafiri kwenda mikoani kukata tiketi katika kampuni husika ili kuepuka kulipa kiasi kikubwa tofauti na bei elekezi.

Hayo yamezungumwa na Afisa Usalama barabarani wilaya ya iringa Koplo Elizabeth na kuongeza kuwa  kila abiria anatakiwa kujua haki na wajibu wake wakati kusafiri ili kuepuka changamoto zinazojitokeza wakati wa safari.

Sauti ya Elizabeth

Aidha Koplo Elizabeth amesema kuwa Abiria anapaswa pia kukemea vitendo hatarishi kwa madereva wanaoendesha gari kwa mwendokasi.

Sauti ya Elizabeth

Kwa upande wake Koplo Fadhili amesema abiria ana haki ya kupewa usafiri mbadala endapo chombo kitakuwa kimepata changamoto wakati wa safari ndani ya masaa mawili.

Sauti ya Koplo Fadhili
Coplo Fadhili akitoa elimu katika kipindi cha Nyambizi Nuru FM