Nuru FM

Takukuru yawanoa wanahabari Iringa

18 October 2025, 8:56 am

Wanahabari Mkoa wa Iringa wakiwa katika Picha ya Pamoja na Mkuu wa Mkoa wa iringa na Mkuu wa Takukuru. Picha na Chacha Robert

“Wanahabari wakielimishwa kuhusu rushwa watatusaidia kutoa elimu kwa wananchi” Swela

Na Joyce Buganda na Adelphina Kutika

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Iringa imeendesha mafunzo maalum kwa waandishi wa habari ili kuwajengea uwezo wa kuelimisha jamii na kuripoti vitendo vya rushwa kuelekea uchaguzi mkuu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo  ya siku moja yaliyofanyika katika ukumbi wa mkoa wa Iringa Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Iringa Bwana victor Swela amewataka waandishi wa habari kutambua nafasi yao muhimu katika mapambano dhidi ya rushwa, hasa katika kipindi nyeti cha uchaguzi. 

Sauti ya Mkuu wa TAKUKURU

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kheri James amewahimiza waandishi hao kuhakikisha wanaripoti viashiria vyovyote vya rushwa mara moja, akisema rushwa ni adui wa maendeleo na haina nafasi katika jamii inayotaka kupiga hatua kimaendeleo.

Sauti ya RC Iringa

Naye Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa (IPC), Frank Leonard, ameipongeza TAKUKURU kwa kuandaa mafunzo hayo, huku akisisitiza kuwa taasisi hiyo ina jukumu la kuhakikisha waandishi wanajengewa uwezo wa kutosha ili waweze kuripoti kwa ufanisi habari zinazohusu uchaguzi na vitendo vya rushwa.

Sauti ya Mwenyekiti IPC

Hata hivyo mafunzo hayo yanatarajiwa kuwapa waandishi mbinu, maarifa na miongozo ya kisheria kuhusu namna ya kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya rushwa, hasa katika muktadha wa uchaguzi unaotarajiwa kufanyika nchini October 29 mwezi huu.