Nuru FM

Madaktari Bingwa kutoa huduma za kibingwa iringa

23 September 2025, 8:00 pm

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kheri James akizungumzia ujio wa madaktari bingwa. Picha na Adelphina Kutika

Na Adelphina Kutika

Madaktari bingwa wapatao 45 kupitia mpango wa Rais Samia Suluhu Hassan wamewasili katika Mkoa wa Iringa kwa lengo la kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakilazimika kusafiri nje ya mkoa iringa  kufuata matibabu.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, amesema ujio wa madaktari hao utasaidia kupunguza gharama za wananchi kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma katika hospitali za kanda na mikoa mingine.

Sauti ya RC

Naye Mratibu wa zoezi hilo kutoka Wizara ya Afya Dkt. Mac Donald  Ulimbakisye amesema wamejipanga kutoa huduma kwa ufanisi mkubwa kwa wagonjwa watakaojitokeza katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.

Sauti ya Mratibu

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Sylivia Mamkwe  amesema huu ni ujio wa awamu ya nne ya madaktari bingwa mkoani humo, ambapo katika awamu ya tatu zaidi ya wananchi elfu mbili walifikiwa na huduma hizo.

Sauti ya Mwamke

Hata hivyo huduma hizo  zinaanza kutolewa September 22 hadi tarehe 26 2025 katika hospitali za wilaya   zilizopo katika Halmashauri tano za  mkoa wa Iringa zikijumuisha fani saba za kibingwa ikiwemo magonjwa ya wanawake na uzazi ,Magonjwa ya ndani,Magonjwa ya kinywa na meno na Upasuaji