Nuru FM

Wanahabari waagizwa kuandika habari zenye tija

22 September 2025, 10:28 am

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Akiwa na wanahabari Iringa. Picha na Adelphina Kutika

“Habari zisizo na maadili huleta taharuki katika Jamii”DC Sitta

Na Adelphina Kutika

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mhe. Benjamin Sitta, amewaagiza waandishi wa habari kutumia mitandao ya kijamii kwa kuandika na kusambaza habari zenye tija kwa jamii, na si zile zinazopotosha umma au kuleta taharuki.

Wito huo umetolewa katika mkutano wa majadiliano kati ya Baraza la Habari (MCT), waandishi wa habari, na maafisa wa serikali, Sitta amesema kuwa mitandao ya kijamii ni silaha yenye nguvu inaweza kujenga au kubomoa, hivyo, waandishi wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha matumizi sahihi ya majukwaa hayo.

Sauti ya DC Sitta

Kwa upande wake   Afisa kutoka MCT  Ziada kilobo amesema majadiliano hayo yamelenga kujadili changamoto zinazowakabili waandishi wa habari, pia kubainisha haki na wajibu wa pande zote zinazohusiana na tasnia hiyo, ili kuweka mizani sawa kati ya waandishi wa habari na mamlaka za serikali.

Sauti ya Ziada

Awali Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa (IPC), Frank Leonard, amesema wanahabari  wanakumbana na madhila mbalimbali ikiwemo hofu inayozuia sauti ya ukweli wa jamii na kupunguza imani ya wananchi kwa vyombo vya habari.

Sauti ya Frank