Nuru FM

Wanafunzi la saba watakiwa kujiamini

10 September 2025, 12:02 pm

Picha ya wanafunzi wakiwa darasani. Picha na Michuzi Blog

Mtihani wa kumaliza elimu ya Msingi unafanyika kuanzia leo Septemba 10 hadi Septemba 11, 2025

Na Noela Lucas na Stephen Gerald

Ikiwa wanafunzi wa Darasa la 7 Nchini wameanza kufanya mitihani ya kuhitimu elimu ya Msingi, wananchi Manispaa ya iringa wamewataka wanafunzi hao wajiamini ili waweze kufanya vizuri.

Wakizungumza Na Nuru fm baadhi ya wananchi wamesema kuwa wahitimu hao wakitakiwa kuendelea kusoma ili wakumbuke kile walichojifunza.

Sauti ya Wananchi

Aidha wamewataka wazazi kuwapa watoto wao nafasi ya kujisomea na kuwapunguzia kazi katika kipindi hiki ambacho wanafanya mitihani yao.

Sauti ya Wananchi

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) Dkt. Said Mohamed amewataka wasimamizi kuhakihikisha watahiniwa wote wanafanya mitihani  kwa muda uliopangwa.

Sauti ya Katibu

Kwa mujibu wa Baraza la NECTA Jumla ya watahiniwa 1,172,279 wameanza kufanya mitihani yao leo.