Nuru FM

Dkt. Samia kujenga Machinga Complex Iringa

8 September 2025, 11:03 am

Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wakazi wa Iringa Uwanja wa Samora. Picha na Ayoub Sanga

Katika Muendelezo wa Kampeni za kunadi sera za Chama Cha Mapinduzi CCM kwa wananchi Mkoani Iringa.

Na Ayoub Sanga

Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza dhamira ya Serikali yake kujenga jengo la kisasa la Machinga Complex Manispaa ya Iringa kabla ya kukamilika kwa kipindi chake cha sasa cha uongozi.

Akizungumza mbele ya maelfu ya wakazi wa Iringa kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika Viwanja vya Samora, Mhe. Samia amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mkakati mpana wa Serikali wa kuboresha mazingira ya kufanyia biashara, hasa kwa wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama wamachinga.

Sauti ya Samia

Mh. Samia amongeza kuwa Manispaa ilifanikiwa kujenza Ofisi za Machinga Mkoa kwa kushirikiana na TAMISEM ambapo lengo kuu ni kuhakikisha wanaondoa changamoto za muda mrefu zinazowakabili wamachinga, zikiwemo uhaba wa maeneo salama ya kufanyia biashara.

Sauti ya Samia

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa CCM, na Mjumbe wa Halmashuri kuu ya Taifa Mkoa Wa Iringa” Salim Abri Asas amesema kuwa watashirikiana na wabunge wa Mkoa wa Iringa kunadi sera za Mgombea wao ili kupata kura za kishindo.

Sauti ya Asas