Nuru FM

Vigogo ACT Wazalendo Iringa wajiuzulu

26 August 2025, 11:56 am

Viongozi wa ACT wazalendo waliojiuzulu Iringa. Picha na Joyce Buganda

ACT wazalendo imekuwa na Mwenendo mbaya wa Uongozi jambo lililopelekea Vigogo wa Chama hicho Jimbo la Iringa kung’atuka” Kalama

Na Joyce Buganda

Viongozi Chama cha ACT wazalendo Jimbo la Iringa Mjini wamejivua uanachama wa chama hicho kutokana na mwenendo mbovu unaoendelea miongoni mwa viongozi wa ngazi ya mkoa.

Hayo yamejili baada ya kuonekana kwa kadi  feki za Chama katika mkutano wa kumteua Diwani wa Kata ya kihesa  ambaye atakiwakilisha chama hicho katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi oktoba mwaka huu

Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa Vijana Chama cha ACT wazalendo  Jimbo la Iringa mjini Dikson Kalama amesema  yeye ameamua kujivua na uanachama kwa sababu chama hicho hakina umoja wala ushirikwishwaji.

Sauti ya Kalama

Baton Larika ni Mweka hazina Chama cha ACT Jimbo la Iringa Mjini amesema amejitoa kwenye chama  viongozi hawashirikishwi toka wachaguliwe.

Sauti ya Laiton

Kwa upande wake Katibu wa ngome ya Wazee Jimbo la Iringa Mjini  Petro Kwanga amemtaka mwnyekiti cha chama cha ACT WAZALENDO mkoa wa Iringa Chiku Abwao kuachia nafasi hiyo kwani haiteendei haki nafasi yake.

Sauti ya Petro

Hata hivyo Katibu Mwenezi wa  Chama cha ACT Wazalendo Jimbo la Iringa mjini  Salehe Chande amesema wapo tayari kukabidhi nyaraka zote za chama cha ACT pia kwa sasa hawatakwnda chama chochote cha siasa.

Sauti ya Chande