Nuru FM

Serukamba aaga Iringa, asisitiza ushirikiano

9 July 2025, 1:43 pm

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kheri James akikabidhiwa Ofisi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huu, Peter Serukamba. Picha na Ayoub Sanga

 
Watumishi na watendaji wote Mkoni Iringa wameaswa kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii kwa uadilifu na uzalendo.

Na Ayoub Sanga

Rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba amekabidhi Ofisi kwa Mkuu wa Mkoa mpya ambae ni Kheri James huku akishukuru kwa ushirikiano aliopewa kipindi alipooongza Mkoa wa Iringa.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya ofisi Serukamba yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa mikutano uliopo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa  amewaasa watuimshi kufanya kazi kwa bidii, kuwa waadilifu wawapo kwenye maeno yao ya kazi.

Sauti ya Serukamba

Aidha Mkuu mpya wa Mkoa wa Iringa Kheri James amemshukuru Mh. Peter Serukamba kwa uongozi wake kwani uongozi wake umewaachia alama kwa watumishi na wananchi wa mkoa wa Iringa.

Sauti ya RC James

Aidha Mhe Kheri James ameahidi kuendeleza juhudi zote ambazo zimekuwepo wakati wote katika usimamizi mzuri kwenye ukusanyaji wa mapato na ukamilishaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa huu

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Iringa Benjamin Sitta amempogeza serukamba kwa uongozi wake lakini pia kwa mheshimiwa Kheri James kwa kuachiwa kijiti anamuamini kwani uongozi wake unajulikana.

Sauti ya DC Sitta

Ikumbukwe kuwa Mheshimiwa Peter Serukamba amehudumu kwa kipindi cha mwaka mmoja na miezi minne na kwa sasa ameingia kwenye siasa.