Nuru FM

RC Heri James asisitiza ushirikiano Iringa

2 July 2025, 4:30 pm

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kheri James akipeana na Mkono na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo. Picha na Godfrey Mengele

Na Godfrey Mengele

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Kheri James amewataka viongozi, Wakuu wa Taasisi na wananchi kwa jumla kuendeleza ushirikiano uliopo ili kutekeleza maendeleo pasina migogoro.

Zoezi la uapisho limefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Iringa ambapo pia viongozi kadhaa wa Serikali na CCM wamehudhuria ikiwemo Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Salim Faraj Abri (Asas)

Akizungumza mara baada ya kuwaapisha wakuu walioteuliwa hiv karibuni wilaya ya kilolo na wilaya ya iringa RC Kheri james amesema kwa kipindi alichohudumu kama mkuu wa wilaya ya iringa kabla ya kupandishwa cheo amepata ushirikiano mkubwa hivyo ni vyema kuendeleza ushirikiano huo.

Sauti ya RC Kheri

Aidha RC Kheri James amezitaka halmashauri zote mkoani iringa pamoja na mamlaka ya ukusanyaji mapato tra mkoa wa iringa kuendelea kukusanya mapato ili kutekeleza shughuli za maendeleo zilizopangwa.

Sauti ya RC Kheri

Katika hatua nyingine mkuu wa mkoa wa iringa kheri james amesema kuwa mkoa wa iringa uko salama na kuwaasha wakuu wa wilaya walioapishwa kutenga muda wa kuwasikiliza wananchi na si kukaa ofisini.

Sauti ya RC Kheri

Wakuu hao wa wilaya ni Benjamin Sitta ambaye ameapishwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Iringa na Estomin Kyando ambaye ameapishwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Kilolo.