Nuru FM

CAHE yawapa tabasamu watoto wenye uhitaji

3 June 2025, 11:45 am

Viongozi wa Taasisi ya CAHE wakiwa na watoto baada ya kuwapatia mahitaji maalumu. Picha na Ayoub Sanga

Taasisi ya CAHE imekuwa ikisaidia na kutatua changamoto za kijamii, hasa zinazowakumba watoto

Na Ayoub Sanga

Taasisi isiyo ya kiserikali ya Caring Hearts (CAHE) imeadhimisha miaka mitatu tangu kusajiliwa kwake kwa kutembelea Kituo cha kulelea watoto yatima na wenye mahitaji maalumu cha Huruma Center kilichopo kata ya Mwangata Manispaa ya Iringa na kutoa mahitaji muhimu

Akizungumza katika tukio hilo, Mkurugenzi wa Shurika la Caring Hearts  Bw. Oswald Kikoti amesema kuwa lengo kuu la taasisi hiyo ni kusaidia na kutatua changamoto za kijamii, hasa zinazowakumba watoto, vijana na wanawake.

Sauti ya Oswald

Kwa upande wake, Mkuu wa kituo cha Huruma Center, Mchungaji Upendo Sanga ameeleza furaha yake kwao ujio wa Caring Hearts na kusema kuwa uwepo wao kituoni hapo umeleta baraka kubwa na faraja kwa watoto.

Sauti ya Mchungaji Pendo

Naye mmoja wa watoto kutoka kituoni hapo Catherine Mwilapwa, kwa niaba ya watoto, ametoa shukrani kwa taasisi hiyo kwa kuwatembelea na kuonyesha upendo, akisema kuwa wamejiona wa thamani mbele ya jamii.

Sauti ya Mtoto

“Tunasema asanteni kwa kutufanya tujihisi kama familia. Mmeleta zawadi, lakini muhimu zaidi mmekuja kutuona. Tumefarijika na tunawaombea Mungu azidi kuwabariki,” amesema Catherine.

Taasisi ya Caring Hearts, iliyosajiliwa mwaka 2022, imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia makundi maalumu katika jamii, kwa kutoa misaada, elimu ya afya ya akili, uwezeshaji wa kiuchumi kwa wanawake na vijana, pamoja na kusaidia waathirika wa ukatili wa kijinsia.