Nuru FM

Madiwani Iringa waagizwa kusimamia ukusanyaji mapato

20 May 2025, 6:25 pm

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba akizungumza katika Baraza la Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Iringa. Picha na Ayoub Sanga

Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imekuwa na mafanikio katika ukusanyaji wa mapato, ikipongezwa kwa kufanya vizuri.

Na Joyce Buganda

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba amelitaka Baraza la madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kusimamia vyema mapato yanayokusanywa na Halmashauri hiyo.

Akizungumza wakati wa kikao Cha Baraza la madiwani kikao Cha robo ya tatu ya kuanzia Mwezi januari mpaka mwezi machi kwa mwaka 2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano  wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba amesema  Halmashauri inatakiwa kutekeleza na kumaliza Miradi kwa wakati ,  kuhakikisha fedha za mikopo zile asilimia 10 zinawafikia walengwa kwa makundi maalumu.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa

“Madiwani fedha hizi ziwafikie wahusika iwe kwa kutengeneza vikundi awe iwe kwa wale wenye vigezo msitengeneze vikundi vyenu “Alisema Serukamba

Kwa upande  wake Mkurugenzi   wa Manispaa ya Iringa Justice Kijazi   amesema  wao kama Halmashauri wamekuwa wakifanya vyema kwenye ukusanyaji wa mapato na wataendelea kufanya hivyo  kwani Halmashauri imekusanya zaidi ya bilioni 6.5 kuanzia mwezi julai 2024 mpaka mwezi Mei 2025 ambayo ni sawa na asilimia 79. 

Sauti ya Mkurugenzi

Hata hivyo Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada amesema watafanya mjadala kujadili sheria ndogo lakini pia wataendelea kusimamia miradi ya maendeleo na kuyafanyia kazi maagizo yote yaliotolewa na mkuu wa Mkoa.

Sauti ya Meya