Nuru FM

Jukwaa la WIW lalaani tukio la udhalilishaji kwa mwanachuo

22 April 2025, 12:27 pm

Makamu wa Rais wa chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Laetitia Petro Ntagazwa akizungumza na waandishi wa Habari Iringa. Picha na Adelphina Kutika

Na Adelphina Kutika

Jukwaa la Wanawake Mawakili na Wanasheria “Wowen Inspire Women” (WIW) linalaani vikali tukio la udhalilishaji lililofanywa na kundi la wanafunzi wa kike dhidi ya mwanafunzi mwenzao wa kike kama lilivyoonekana kupitia picha mjongeo iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Akizungumza  na vyombo vya habari mjini Iringa Makamu wa Rais wa chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Laetitia Petro Ntagazwa amesema  Wowen Inspire Women ni jukwaa  huru lililoanzishwa kwa lengo ni  kusaidiana wanawake mawakili na wanasheria kusaidiana kupeana sapoti katika mambo yanayowakabili wenyewe na wanawake nchini

Sauti ya Wakili

“Tukio hili si tu linakiuka misingi ya utu na heshima ya binadamu, bali pia linaashiria kukosekana kwa maadili, nidhamu, na uelewa wa sheria miongoni mwa baadhi ya wasomi vijana wa leo,” alisema Ntagazwa.

Katika hatua nyingine amepongeza”WIW” kwa hatua za haraka zilizochukuliwa na Serikali kupitia kwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, hasa kwa kuhakikisha manusura anapata msaada wa kisaikolojia, kisheria, na kijamii.

Sauti ya Wakili

Aidha amesema tukio lingine limetokea March 21 2025 katika wilaya mufindi eneo la Bagdadi Mkoani Iringa wanawake wanne walimshambulia mwanamke mwezao na kumjeruhi kupita kiasi kwa tuhuma za wivu wa kimapenzi.

Sauti ya Mwanasheria