Nuru FM

DC Kheri aiagiza TAWA kudhibiti wanyamapori wanaovamia mazao ya wananchi

7 March 2025, 6:36 pm

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Kheri James akizungumza kuhusu utaratibu wa kuwadhibiti wanyama waharibifu. Picha na Godfrey Mengele

Na Godfrey Mengele

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Kheri James ameitaka Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania – TAWA pamoja na hifadhi ya wanyamapori Ruaha kuchukua hatua madhubuti ili kudhibiti wanyama wanaovamia na kuharibu mazao, mifugo na kusababisha madhara kwa binadamu

DC Kheri James ametoa maagizo hayo kwenye kikao cha ushauri cha Wilaya kilichofanyika Ofisini kwake na kueleza hivi karibuni kuna baadhi ya vijiji vilivyopo karibu na hifadhi na mapori tengefu vimevamiwa na wanyama hao ikiwamo simba na tembo na kufanya uharibifu ambapo ng’ombe 9 zimeliwa .

Sauti ya DC

Kheri James amewataka wananchi kutoa taarifa ikiwa uvamizi wa wanyama utaendelea katika maeneo tofauti na kuziagiza mamlaka husika pindi wapatapo taarifa wazifanyie kazi haraka ili kuzuia madhara makubwa kutokea.

Sauti ya DC

Aidha Kheri James amewataka wananchi kujenga tabia ya kutunza mazingira ili kufanya mfumo wa ikolojia kubaki salama na kuepuka madhara ya wanyama waharibifu wanaovamia na kuharibu mali za watu kama mazao na mifugo

Sauti ya DC

Msikilizaji taarifa hii utaisikia kwa kina hapo baadae ambapo atasikika Afisa tarafa, tarafa ya idodi Ndg Mapesa Makalla akitueleza hatua ambazo wamezichukua ili kukabiliana na changamoto hiyo.

Sauti ya Afisa

MWISHO