Nuru FM

Wanawake Iringa washauriwa kuacha mikopo ya kausha damu

5 March 2025, 10:15 am

Mkurugenzi mtendaji wa shirika la Vyombo vya Habari kwa Maendeleo ya Jamii Rose Ngunangwa akizungumza katika Kongamano Mkoani Iringa. Picha na Adelphina Kutika

Na Adelphina Kutika

Wanawake Mkoani Iringa  wametakiwa kuacha kukopa mikopo ya kausha damu na badala yake wakope mikopo inayotambulika na Serikali ikiwemo taasisi za fedha ili kupunguza vifo kwa vijana.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa shirika la Vyombo vya Habari kwa Maendeleo ya Jamii Rose Ngunangwa , katika Kongamano la Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani lililoandaliwa na shirika la Sauti ya Haki Tanzania na kufanyika katika Ukumbi wa Mwananchi Uliopo Kata Nduli Manispaa Ya Iringa na kuwashauri wanawake wanapokopa wahakikishe wanafanyia malengo yaliyokusudiwa.

Sauti ya Mkurugenzi

Letsia Petro Ntagazwe ni mkurugezi wa shirika la sauti ya haki Tanzania amesema kuwa kama shirika wameona vyema waadhimishe siku ya mwanamke  katika kata ya nduli ili kumfikia mwanamke wa chini asiyeitambua haki yake.

Sauti ya Letisia

Kwa upande wake Paskalina Johel Ipanda Program manager sauti ya haki Tanzania amesema  kupitia  changamoto zote zilizotolewa katika kongamano hilo zinakusanywa na kufanyiwa kazi ili kutoa suluhisho la kudumu kwa wanawake wa hali ya chini

Sauti ya Paskalina

Nao baadhi ya wanawake waliohudhuria maadhimisho hayo wamesema mikopo kausha damu imekuwa mibaya kutokana na kutumia pasipo malengo hali inayopelekea wanaume kufariki.

Sauti ya Wanawake

Hata hivyo maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka 2025 yatakuwa kwa namna ya kipekee yakibeba sura ya kipekee kwa kuwa yanaambatana na miaka 30 ya utekelezaji wa Azimio la ulingo wa Beijing (1995) yakiambatana na  kaulimbiu isemayo “Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji”

MWISHO