Nuru FM

Tume ya haki za binadamu yatoa elimu kwa wananchi

19 February 2025, 12:24 pm

Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora Dkt. Thobias Masanja akiwa na wanahabari Iringa. Picha na Adelphina Kutika

Na Adelphina Kutika

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora Nchini inatarajia kutoa elimu kuhusu misingi ya haki na Utawala bora kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Iringa kwa lengo la kuwawezesha Wananchi kutambua haki zao na kudumisha Utawala unaozingatia haki za binadamu.

Hayo yamebainishwa na Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora Dkt. Thobias Masanja  wakati Akizungumza na Vyombo vya Habari katika ofisi ya Mkoa wa Iringa kuhusu zoezi la kutoa elimu kwa wananchi katika Halmashauri mbalimbali za Mkoa wa Iringa.

Sauti ya Kamshina

Masanja ameeleza kuwa mikutano hiyo itatumika kuitambulisha Tume kwa wananchi, kuwaskiliza na kupokea malalamiko yao yanayohusu haki za binadamu na utawala bora katika maeneo yao.

Aidha, Dkt. Masanja amesema kuwa elimu ya misingi ya haki za binadamu na utawala bora itatolewa kwa wanafunzi katika shule za sekondari na vyuo mbalimbali, ili kuwajengea uelewa na kuwaandaa kwa mustakabali wa kuwa viongozi bora katika siku zijazo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Iringa Press clabu Frank Leonard ameipongeza tume hiyo kwa kufika mkoani Iringa  kuja kitoa elimu kwa jamii juu misimgi ya utawala bora pamoja na kutambua haki zao.

Sauti ya Mwenyekiti

Aidha, zoezi hilo litaambatana na kutembelea Magereza za Mkoa hapa kwa lengo kukagua na kutathmini haki za watu wanaozuiliwa, na kutoa mapendekezo jinsi ya kutatua matatizo yaliyopo kwa mujibu wa taratibu na Sheria zilizopo ikiwa ni pamoja na kukagua viwango vya kimataifa na kikanda vinavyolinda na kutetea haki za binadamu ikiwemo makundi ya watu waliozuiliwa.

MWISHO