Nuru FM

RC Serukamba aagiza kutendeka haki katika huduma za kimahakama

5 February 2025, 11:48 am

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba akizungumza katika wiki ya Sheria. Picha na Joyce Buganda

Na Joyce Buganda

Wadau wa mahakama mkoani iringa wametakiwa kutenda haki wanapokuwa katika majukumu yao ikiwemo kujenga ukaribu kwa wananchi wakati wa wanapotoa huduma za kimahakama.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya  kilele cha  siku ya sheria yaliofanyika katika viwanja ya mahakama mgeni rasmi wa maadhimisho hayo mkuu wa mkoa wa iringa Peter Serukamba amesema  jamii pamoja na wadau wa mahakama washirikiane kwa pamoja katika kutokomeza rushwa haki itendeke.

Sauti ya RC

Aidha Mwenyekiti wa Chama cha Mawakili TLS kanda ya Iringa Moses Ambindwile amesema mawakili wa kujitegemea wamekuwa wakipata changanoto nyingi ikiwemo kupewa maneno makali mbele za wateja wao kutoka kwa wadau wa mahakama.

Sauti ya TLS

Kwa upande wake jaji mkuu mahakama kuu kanda ya Iringa  Dustan Ndunguru  amesema maadhimisho hayo yalijumuisha utoaji wa elimu kuhusu sheria kupitia vyombo mbalimbali vya habari kama radio, television ana kwa ana.

Sauti ya Jaji

Ikumbukwe kauli mbiu ya  mwaka huu inasema Tanzania 2050 nafasi ya Taasisi zinazosimamamia haki, madai katika kufikia malngon makuu ya Dira ya Taifa ya maendeleo.