Nuru FM

Shirika la USAID latoa vifaa na zana za kilimo kwa Vijana 50 Iringa

19 September 2024, 7:51 pm

Naibu Waziri  Ofisi ya Waziri  Mkuu  , Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu   Patrobas Pascal Katambi akizungumza na Vijana wanaopatiwa msaada wa Vifaa na zana za kilimo Mkoani iringa. Picha na Hafidh Ally

Na Adelphina Kutika

Shirika la marekani la maendeleo ya kimataifa,kupitia mradi wa feed the future Tanzania imarisha sekta binafsi (PSSP) limekabidhi vifaa na Zana za kilimo kwa vijana (50) wajasiriamali wanajishughulisha kilimo biashara Mkoani  iringa.

Akizungumza aliyekuwa mgeni rasmi wa hafla ya hiyo Naibu Waziri  Ofisi ya Waziri  Mkuu  , Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu   Patrobas Pascal Katambi amewataka vijana hao kuitumia fursa hiyo vizuri pamoja  kutunza vifaa walivyokabidhiwa ili kujikwamua na wimbi la umasikini.

Sauti ya Naibu Waziri

Rais  wa Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC) CPA Mercy Sila, Katika hotuba yake  ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  katika ngazi zote kwa juhudi zinazofanywa za kuweka mazingira wezeshi yatakayowasaidia vijana  kujikwamua kiuchumi .

Sauti ya Mercy

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada amesema kama Halmashauri na Mkoa kwa ujumla watahakikisha wanasimamia pesa zinazotoka halmashauri kuu ili vijana wanufaike na pesa hizo.

Sauti ya Meya

Awali  Mkurugenzi wa Feed the Future Tanzania Imarisha Sekta binafsi Edward Furaha amesema  wamegusa zaidi vijana ili kuongeza fursa za kiuchumi  pamoja na kukamilisha lengo la kisera la kuwapatia mitaji na mikopo.

Sauti ya Edward

Aidha mkirugenzi wa Pass Leasing   Company  Killo lusewa amesema kuwa lengo kuu la Pass leasing company ni kuwawezesha vijana  katika sekta ya kilimo kwa kuwapatia mashine na zana za kilimo,uvuvi na ufugaji.

Sauti ya Killo

Kwa upande wao vijana wanaonufaika  mradi wa feed the Future Tanzania  chini ya ufadhili wa shirika la Marekani la Maendeleo ya kimataifa (USAID) wameshukuru mradi huo kwa kuwawezesha vifaa ambavyo vitawasaidia kujikwamua kiuchumi.

Sauti ya Wanufaika

Hata hivyo Feed the Future Tanzania Imarisha Sekta binafsi ni mpango wa Kimataifa wa kudhibiti njaa na usalama wa chakula wa serikali ya marekani kwa kuzingatia  wakulima wadogo hasa wanawake.

MWISHO