Nuru FM

CAMFED kuja na filamu kuhamasisha elimu kwa mtoto wa kike

26 August 2024, 10:06 am

Mratibu wa Camfed akizungumza kuhusu filamu itakayohamasisha wananchi kuwapa elimu watoto wa kike. Picha na Ayoub Sanga

Elimu ya watoto wa kike ni moja ya njia bora za kupunguza umaskini, mimba na ndoa za utotoni katika mataifa yanayostawi.

Na Adelphina Kutika

Wadau wa elimu mkoani Iringa wamelitaka shirika la Campaign for Female Education (CAMFED) kuisambaza kwenye jamii na maeneo ya shule za bweni  filamu ya “Tunainuana” iliyoandaliwa  na mwazilishi wa mtandao wa Wasichana Wasomi wa Africa hapa nchini Bi Lydia Wilbard ili kuleta mabadiliko chanya katika kumuelimisha mtoto wa kike.

Akizungumza mara baada ya hafla ya kutizama filamu hiyo, Afisa Vijana wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Bw. Hamis Sabuni amesema filamu hiyo ikipelekwa kwenye jamii itabadilisha mitizamo ya wazee vijijini wanaoamini mtoto wa kike hapaswi kupata elimu.

Sauti ya Afisa Vijana

Mratibu wa CAMFED Wilaya ya Iringa Vijijini Maua Omary,  amesema kuwa lengo la kuonesha filamu hiyo ni kuonyesha jinsi mtoto wa kike anavyoweza kushinda changamoto zinazomkabili na kufikia malengo yake.

Sauti ya Mratibu CAMFED

Winnie Oscar Boaz, mmoja wa wananchi walioshiriki hafla hiyo, amesema kwamba amejifunza kuwa mtoto wa kike akiwezeshwa kielimu anaweza kujitambua na kutimiza ndoto zake.

Sauti ya Boaz

Baadhi ya wanaCAMA waliohudhuria hafla hiyo wameeleza kuwa filamu hiyo imewafundisha namna ya kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kumuelimisha mtoto wa kike

Sauti ya Wanacama

MWISHO