Nuru FM

Wakurugenzi Iringa kutenga bajeti ya program ya malezi PJT MMMAM

14 August 2024, 8:20 am

Wakuu wa Idara kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa na watekelezaji wa Program ya PJT MMMAM wakiwa katika picha ya pamoja. Picha na Joyce Buganda

Utekelezaji wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto ( PJT-MMMAM) unaweza kutoa suluhisho la kudumu la changamoto inayokabili mkoa wa Iringa ya ukatili wa kijinsia, lishe, afya na malezi bora dhidi ya watoto hususan walio kati ya umri wa miaka 0 hadi 5.

Na Joyce Buganda

Wakuu wa wilaya mkoani Iringa wametakiwa kuendelea kusimamia  kikamilifu utendaji wa programu jumuishi ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto PJT MMMAM hasa kwenye ngazi ya jamii kuhakikisha elimu hii inawafikia walengwa kwa afua zote tano.

Akizungumza katika kikao cha tathmini  ya programu jumuishi  ya taifa  ya malezi makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto PJT MMMAM kwa ngazi ya mkoa Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa iringa Venance Ntyagundura  ambae alimuwakilisha mkuu wa mkoa wa Iringa amesema ni vema Wakurugenzi wa Halmashauri watenge bajeti ili kuwezesha utekelezaji wa program hii.

Sauti ya Katibu Tawala

Aidha ni afisa ustawi wa mkoa wa iringa ambae pia ni mratibu  wa PJT MMMAM kwa mkoa wa iringa Martin Chuwa  amesema wanajitahidi kuwafikia makundi tofauti tofauti ili kutoa elimu kuhusu program hiyo.

Sauti ya Chuwa

Hata hivyo mwandishi kinara wa habari za watoto mkoani iringa Tukuswiga mwaisumbe amesema zaidi ya watu 1000 wamefikiwa kupitia vyombo vya habari kwa mkoa wa iringa kwa kupitia vipindi, makala  na habari.

Sauti ya Mwaisumbe

Kwa upande wao baadhi ya wadau walioshiriki kikao hicho wamesema wameshuru kupata elimu hiyo kwanin kumewafanya wakawe mabalozi na walimu kwa wenzao.

Sauti ya wadau

PJT MMMAM ni program jumuishi ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kuanzia miaka 0 mpaka miaka 5 ambayo ina afua tano ambazo ni afya bora, malezi, lishe, elimu na ulinzi na usalama kwa mtoto.

MWISHO