Nuru FM

Wakazi wa Jimbo la Isimani waagizwa kujiandikisha daftari la mpiga kura

13 August 2024, 10:13 am

Katibu wa Mbunge wa jimbo la Ismani Amos Ndaso akizungumzia kuhusu ushiriki wa vijana katika uchaguzi wa serikali za Mitaa. Picha na Adelphina Kutika

Na Adelphina Kutika

Wakazi  wa kata ya Malengamakali, Jimbo la Isimani, wilaya ya Iringa, wametakiwa  kujiandikisha  katika daftari la mpiga kura ili waweze kushiriki zoezi la uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi Mkuu mwakani.

Wito huo umetolewa na Afisa Tarafa wa Jimbo la Isimani, Thomas Myinga, wakati  akizungumza na wananchi  wa kijiji cha Iguluba na Usolanga  ambapo ameeleza kuwa wanaopaswa kujiandikisha ni wale wenye umri wa miaka 17 na waliohama makazi.

Sauti ya Myinga

Kwa  upande wao  makatibu wa Jimbo la Isimani ,Israel Chotamasege na Amos Ndaso , wamesema wananchi wanatakiwa kuboresha taarifa zao kwenye daftari la mpiga kura ili kupata nafasi ya kupiga kura na kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.

Sauti ya Ndaso na Chotamasege

Mwenyekiti wa kijiji Cha Iguluba benitho Garus Mkisi amewataka vijana kuhakikisha wanadumisha upendo na amani kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.

Sauti ya Mwenyekiti

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unahusisha kuchagua viongozi kwenye nafasi za Mwenyekiti wa Kijiji, Mwenyekiti wa Kitongoji, Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji (Mchanganyiko) na Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji (Kundi la Wanawake).

MWISHO