Nuru FM

DC Linda ahimiza mkakati wa kutokomeza ukatili na udumavu Mufindi

16 July 2024, 11:47 am

Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Dkt Linda Salekwa akizungumza na wakazi wa Wilaya hiyo kuhusu Ukatili na udumavu. Picha na Joyce Buganda

Kutokana na kuwepo kwa matukio ya ukatili, Wilaya ya Mufindi imeweka mkakati wa kukabiliana na changamoto hiyo ili kukuza ustawi katika wilaya hiyo.

Na Joyce Buganda

Serikali wilaya ya Mufindi imewataka wazazi na walezi Wilayani Humo kuhakikisha wanapambana na matukio ya ukatili wa kijinsia na kupambana na udumavu ili kukuza ustawi wa jamii.

Hayo yamezungumzwa na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Dkt. Linda Salekwa   katika ziara ya kikazi kwenye Vijiji vya Kipanga, Ilogombe, Mapanda, Uhafiwa, na Katika Bwawa la Uzalishaji wa Umeme Kihansi na kuongeza kuwa jukumu la malezi ni la wazazi.

Sauti ya DC Linda

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mapanda Obadia Kalenga amesema kuwa ziara ya mkuu wa wilaya imeleta matunda kwani wameazimia kutumia fedha za wananchi kukamilisha miradi ya maendeleo sambamba upatikanaji wa bima za afya kwa wananchi wao.

Sauti ya Diwani

Mkuu wa  wilaya ya mufindi anaendelea na ziara wilayani humo ambapo atatembelea miradi ya maendeleo pamoja na kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

MWISHO