Nuru FM

Omoti: Msipandishe nauli kwa wanafunzi

3 July 2024, 8:42 am

Picha ya Miongoni mwa mabasi yanayotumiwa na wanafunzi. Picha kwa msaada wa mtandaoni

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imesema itawachukulia hatua za kisheria  mabasi yanayotoa huduma ya usafiri kwa wanafunzi kuacha tabia ya kupandisha nauli.

Na Godfrey Mengele

Kampuni za Usafirishaji Abiria Mkoani Iringa zimetakiwa kutopandisha nauli kipindi hiki ambacho shule zimefunguliwa ili kuepukana na faini.

Akizungumza na kituo hiki Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya usafiri wa Ardhini Latra Mkoa wa Iringa Joseph Omoti amesema kuwa wingi wa abiria au kuongeza kwa wahitaji wa usafiri isiwe sababu ya kukiuka bei elekezi zilizowekwa na mamlaka hiyo

Sauti ya Omoti

Aidha Omoti amezikumbusha shule kuzingatia taratibu wanazopaswa kuzifuata katika vyombo vyao vya moto kipindi hiki shule zikiwa zimefunguliwa.

Sauti ya Latra

Pamoja na Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya usafiri wa Ardhini Latra Mkoa wa Iringa Joseph Omoti amezitaka shule zinazo wakusanya watoto na kuwachukua kwa magari binafsi kuhakikisha madereva kupitia vyombo hivyo wanakuwa na kibali cha kusafirisha abiria.

Sauti ya Omoti

MWISHO