Nuru FM

Manispaa ya Iringa kuendesha kliniki ya kutatua migogoro ya ardhi

12 June 2024, 9:45 am

Watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wakiwa katika uzinduzi wa kliniki ya ardhi Kata ya Nduli. Picha na Adelphina Kutika

Mara nyingi migogoro midogo midogo ya ardhi isiposhughulikiwa kikamilifu na dalili zake kupuuzwa hugeuka kuwa migogoro mikubwa jambo lililopelekea Halmashauri ya manispaa ya Iringa kuanzisha kliniki ya ardhi kwa wakazi wake.

Na Adelphina Kutika

Wananchi wa kata ya Nduli Halmshauri ya Manispaa ya Iringa wametakiwa kurasimisha ardhi  ili kumaliza migogoro ya ardhi  inayojitokeza katika kata hiyo.

Agizo hilo limetolewa na mstahiki meya Ibrahimu Ngwada Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Iringa katika uzinduzi wa kliniki ya ardhi inayondelea katika kata ya Nduli  ambapo  pamoja na kutatua migogoro ya ardhi , wananchi  pia wamekabidhiwa  hati za umiliki wa ardhi watakazotumia katik shughuli mbalimbali za maendeleo.

Sauti ya Meya

Kwa upande wake  Afisa ardhi  wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Abenance Kamomonga amesema kuwa changamoto waliyoibaini katika  kliniki hiyo  ni uelewa mdogo  wa elimu ya urasimishaji ardhi hali inayopelekea  wananchi kuwa na malalamiko  na sio migororo.

Sauti ya afisa Ardhi

Nae diwani wa kata ya Nduli Bashiri Mtove ameomba  vipande vyote vipimwe pamoja na kurasimisha ili kuondoa migogoro katika kata hiyo.

Sauti ya Mtove

MWISHO