Nuru FM

One Acre Fund yatoa miti mil 2.6 Nyanda za Juu Kusini

7 June 2024, 12:41 pm

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba akiwa na watendaji wa One acre Fund kuzungumzia kuhusu Mpango wa Taasisi hiyo. Picha na Joyce Buganda

Upandaji na uwepo wa misitu katika jamii zetu unachangia asilimia 47 ya akiba ya hewa ukaa ya misitu duniani na hutoa asilimia 60 ya miti ya mbao inayotumiwa viwandani duniani.

Na Joyce Buganda

Zaidi ya miti milioni 2 na laki 6 imesambazwa na kupandwa kutoka kampuni ya One Acre Fund kwa wakulima wa mikoa ya Iringa, Njombe, Mbeya na  Songwe katika msimu wa mwaka 2023 na 2024 ili kutunza mazingira na kukuza kipato.

Akizungumza wakati walipowatembela wakulima katika kijiji cha utengule kata ya Ihimbo wilaya ya Kilolo Afisa Habari kutoka kampuni ya One Acre Fund  Dorcas Tinga amesema kwa kipindi cha miaka mitatu wakulima ambao watatunza miti yao vizuri watapewa motisha kwa kila mti.

Sauti ya AFISA HABARI

Aidha Christina mgata ambae ni Afisa Carboni wa kampuni ya ONE ACRE FUND amesema mradi huo unatoa miti ya aina nne pia miti hiyo ina faida nyingi ikiwemo kurutubisha udongo.

Sauti ya Mgata

Hata hivyo baadhi ya wakulima wamesema wanaishukuru kampuni hiyo kwa kuwapa  mafunzo pamoja na miti kwani kumewafanya wawe walimu kwa wenzao.

Sauti ya wakulima

Awali mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba wakati akiongea na viongozi wa kampuni  ya ONE ACRE FUND  aliwashukuru  kwa kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha  kilimo mseto  ambacho  ni rafiki wa mazingira  pamoja na kutoa elimu  ambazo zinasaidia  kuhifadhi mazingira  na kurutubisha udongo.

Sauti ya RC Iringa

MWISHO