Nuru FM

Wananchi Iringa waomba serikali kuingilia kati mgogoro wa ardhi

5 June 2024, 12:22 pm

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Kheri James akizungumza na Wananchi wa Tarafa hizo kuhusu mikakati ya kutatua Migogoro ya ardhi. Picha na Adelphina Kutika

Migogoro ya ardhi imetajwa kuwa sababu ya Wananchi Wilaya ya Iringa kutokuwa na maelewano.

Na Adelphina Kutika

Wananchi wa Tarafa za Idodi na Tarafa ya Kiponzero  iliyopo ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wameiomba Serikali kutatua changamoto ya Mgogoro wa ardhi inayopelekea wananchi kupigana.

Hayo yamezungumzwa na Wenyeviti wa vijiji vya Tarafa hizo na kuongeza kuwa wakulima walivamiwa  na  wananchi  wa idodi  hali inayosababisha kuharibu mazao ya wakulima huku wakiiomba serikali kuingilia kati.

Sauti ya Wenyeviti

Awali Diwani wa Kata ya Kihanga Khamis Sabuni Nziku amesema toka alivyoingia madarakani changamoto inayowakabili ni mgogoro wa ardhi hali inayopelekea wananchi kutokuwa na maelewano.

Sauti ya Diwani

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iringa Kheri James amewaagiza wataalamu wa ardhi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Vijijini  kushughulikia kero ya ardhi katika tarafa ya Idodi na Tarafa ya Kiponzero  iliyopo ndani ya Halmashauri hiyo na kupeleka mrejesho  ndani ya siku saba.

Sauti ya DC Kheri

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya ameagiza wataalamu kuwa na utaratibu wa kukagua miradi ya maendeleo pamoja na kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili wananchi wa Kata ya Kihanga,Wasa na Maboga zilizopo  katika Halmashauri hiyo.

MWISHO